CategoriesJobsLegal

17.01.2022Tanzania, Dar Es Salaam

USAJILI WA KAMPUNI

Negotiable

Description

Mambo ya kuzingatia i. Kwanza, kampuni husajiliwa na watu kuanzia wawili. Mtu mmoja huwezi kusajili kampuni. Watu hao huitwa wanahisa. Wanahisa hugawana hisa kulingana na mchango wa kila mmoja katika kuanzisha kampuni na biashara husika. ii. Kampuni pia lazima iwe na wakurugenzi kuanzia wawili na kuendelea. Hawa ndio wataunda bodi ya wakurugenzi ya kampuni. iii. Ili kuwa mwanahisa lazima uwe na umri kuanzia miaka kuanzia 18 na ili kuwa mkurugenzi lazima uwe na umri wa miaka kuanzia 21. iv. Unaweza kuwa mwanahisa na mkurugenzi, mwanahisa bila kuwa mkurugenzi au kuwa mkurugenzi bila kuwa mwanahisa. v. Sheria inaruhusu wanahisa au wakurugenzi kuwa wana familia (mfano, baba, mama na watoto) vi. Ni vizuri kufanya uchaguzi sahihi wa watu wa kufungua kampuni nao. Maana kukiwa na migogoro ya mara kwa mara itaua kampuni. Mahitaji i. Kila mwana hisa atatakiwa kuwa na vitu vifuatavyo • Awe na namba ya kitambulisho cha uraia (NIDA), kama ni mgeni awe na passport. • Awe na namba ya simu, awe na barua pepe, awe na anuani ya posta na anuani ya makazi ii. Kila mkurugenzi anatakiwa kuwa na vitu vifuatatvyo • Awe na namba ya kitambulisho cha uraia (NIDA) Kama ni mgeni, awe na passport. • Awe na namba ya mlipa kodi (TIN), awe na namba ya simu, awe na barua pepe • Awe na anuani ya posta na anuani ya makazi iii. Pendekezeni jina la kampuni iv. Pendekezeni mtaji wa kampuni v. Onyesheni mgawanyo wa hisa Hatua za usajili i. Hatua ya kwanza ni kufungua akaunti ya usajili katika mfumo wa usjili wa Brela. ii. Hatua ya pili ni kuandaa nyaraka za usajili. Nyaraka hizo ni memorandum and articles of association, Form namba 14b na form ya maadili. iii. Hatua ya tatu ni ni kuingiza maombi yako mtandaoni katika akaunti yako ya usajili iliyo katika mfumo wa usajili wa Brela iv. Kufanya malipo ya serikali. v. Usaliji kukamilika. Gharama za usajili. Kuna gharama za aina mbili. Gharama za serikali na gharama zetu (Consultancy fee). Gharama za serikali hubadilika kadiri mtaji unavyobadilika. Mfano, ukisajili kampuni ya mtaji wa million 20, gharama za serikali ni 332,200/=. Tutakupatia control number utalipa mwenyewe. Gharama zetu (Consultancy fee). Ni 350,000/= tu

IMMORTAL CONSULTING COMPANY

Member since 2022.
xxx xxx xxx xxx

User

Categories

Location

Dar Es Salaam