Description
Microfinance ni sekta ndogo changa ndani ya sekta ya fedha. Ni sekta ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikijiendesha bila sheria wala kanuni, ,paka miaka ya hivi karibuni. Kwa sasa, kampuni za mikopo zinaongozwa na sheria ya huduma ndogo za fedha (Microfinance Act). Sheria hiyo imeipa mamlaka benki kuu ya Tanzania kutoa leseni na kusimamia kampuni za mikopo. Benki kuu ya Tanzania ilitunga kanuni za microfinance ambazo zinaeleza mahitaji, taratibu za kufuata na mambo ya kuzingatia ili mwobaji aweze kupata leseni ya Microfinace. Itakuwa jambo la busara kwa anayetaka kufanya biashara hii kupata kanuni hizo na kuzisoma. Kwa lengo la kuleta uelewa mpana wa jambo hili, nitaeleza hatua nne kuu za kuanzisha kampuni ya mikopo. Hatua ya kwanza: Kusajili kampuni itakayokuwa inafanya biashara ya Microfinance. Hapa utafuata utaratibu wa kawaida wa kusajili kampuni, japo kuna masharti ya ziada ya kuzingatia wakati wa kusajili kampuni hiyo kama kiwango cha mtaji (Share Capital) kisichopungua million 20, n.k Kazi hii hufanyika BRELA. Katika hatua hii, kuna gharama za serikali na gharama za kwetu (consultancy fee) kama tutakufanyia kazi hiyo. Gharama za serikali hubadilika kulingana na mtaji (sharecapital) inayosajiliwa. Mfano, kampuni ya mtaji wa 20 Million, gharama zake ni 346,000 na kampuni ya mtaji wa 50 Million gharama zake ni 512,000/= kwa upande wa gharama zetu (consultancy fee) ni 350,000/= tu. Hatua ya pili: Hatua ya Pili ni kupata TIN ya kampuni, hili ni zoezi la siku moja tu, na hufanyika katika ofisi za TRA zilizo karibu nawe. Andaa mkataba wa pango wenye mhuri wa mwanasheria, barua ya serikali ya mtaa na ujaze form za TIN. TIN ni bure, japo kuna kodi ya pango (withholding Tax 10%) na Stamp duty 1%. Utalipa hizo ili upewe Tax clearance ya kampuni. Hatua ya tatu: Hatua ya Tatu ni kufanya maombi Leseni ya Microfinance inayotolewa na Benki kuu ya Tanzania. Hapa kuna mambo mengi ya kufanya, kuna nyaraka nyingi za kuandaa na zinahitaji umakini na weledi mkubwa. Kuna mambo kadhaa ambayo mwombaji anatakiwa kuwa nayo, nitayataja uchache. - Mwombaji awe na Sera ya Mkopo - Mwombaji awe na uthibitisho wa uwepo wa mtaji - Mwombaji awe na uthibitisho wa namna mtaji ulivyopatikana kihalali - Bodi ya wakurugenzi wenye sifa - Ripoti za wakurugenzi kutoka credit reference bureau - Nyaraka mbalimbali za kampuni - Nyaraka za kisheria kama viapo - Nyaraka mbalimbali za wakurugenzi Gharama katika hatua hii ni gharama za serikali ambazo ni Tsh 500,000/= Hakuna muda maalmu wa leseni kutoka, inategemea na BOT wenyewe. Tunachoweza kufanya ni kuwakumbusha pale tunapoona muda mrefu umepita. Hatua ya nne: Hatua hii ni kufanya maombi ya leseni ya biashara. Hii ni leseni inayotolewa na Brela. Inachukua siku tano kupatikana na gharama za serikali ni Tsh 600,000/= Kwa ushauri na huduma, wasiliana nasi